Mchaka Zaidi

Saturday, April 25, 2015

Udampo wa Bidhaa za nje Anguko la Shilingi ya Tanzania

 
Shilingi ya Tanzania itaendelea kuporomoka kila mara endapo nchi itaendelea kutegemea bidhaa toka nje kwa kiwango kikubwa kuliko inavyozalisha ndani.
 
Akizungumza na MPEKUZI Profesa Prosper Ngowi toka Chuo Kikuu cha Mzumbe alisema watanzania wasitegemee miujiza wa kukua kwa uchumi wa nchi yao endapo nchi itaendelea kuwa dampo la bidhaa toka nje ya nchi.
 
Alisema Tatizo kubwa la Tanzania ya leo ni kukubali kwake kutumiwa kama dampo la bidhaa nyingi toka mataifa ya nje, tena nyingi ya bidhaa hizo zikiwa feki zisizio kuwa na viwango.
 
Alisema hali imezidi kuwa mbaya katika miaka ya hivi karibuni baada ya Tanzania kuridhia masuala ya soko huria.
 
“Hebu angalia hata baadhi ya huduma za kijamii hapa nyumbani leo zinapatikana kwa kutumia dola suala linalochangia kuiporomosha thamani ya shilingi yetu” alisema Profesa Ngowi.
 
Alisema njia pekee inayoweza kuiokoa shilingi ya Tanzania ni nchi kuanza kuwekeza katika uzalishaji wa bidhaa za ndani ili mwisho wa siku tuweze kuuza nje kwa wingi.
 
“Haiwezekani ukakubali kugeuka dampo la bidhaa nyingi tena mbovu toka nje halafu utarajie dhamani ya fedha yako ikawa juu hiyo haiwezekani” alisema Profesa Ngowi.
 
Alisema hata mamlaka husika nazo kwa kiwango kikubwa zimekuwa zikichangia kwa kiwango fulani kuporomoka kwa dhamani ya shilingi yetu kwa kuruhusu bidhaa kuingia nchini kiholela.
 
Alisema nilazima tuwe makini na baadhi ya sera tunazoletewa na wenzetu toka nje kwani mara nyingi huwa zinalenga kutumaliza ili tuendele kuwa tegemezi toka kwao.
 
Alisema wakati Tanzania inapata uhuru wake viongozi walihimiza sana nchi kuzalisha ndani kwa maana ya kuiwezesha nchi kupata fedha za kigeni kwa wingi.
 
“Hali hii ilikuja kubadilika mara baada ya kuletewa mashariti ya kiuchumi nasi tukayapokea bila hata ya kujiuliza madhara yake ya baadae” alisema Profesa Ngowi.
 
Alisema kama nchi inatakiwa tuache kufikiria ndoto za alinacha kuwa uchumi wa nchi unaweza kukua kwa kwa nchi kuendelea kuwa dampo la bidhaa toka nje ya nchi.
Mpekuzi blog

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.