Mchaka Zaidi

Saturday, April 25, 2015

Serikali Yaanza Tathmini Kero za Muungano

 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais( Muungano) Samia Hassan Suluhu amesema kero mbalimbali za Muungano zilizoibuliwa zimeanza kufanyiwa tathmini na Serikali.
 
Suluhu alisema hayo  jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa wakati alipokuwa akizindua onesho la miaka 51 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
 
Alisema moja ya hatua zilizoanza kuchukuliwa na Serikali juu ya kero hizo ni kuyaingia baadhi ya masuala ya Muuungano katika Katiba Inayopendekezwa kwa lengo la kuyatambua.
 
“Kutokana na kuibuka kwa kero hizo, Serikali ilikaa na kufanya tathmini na ndiyo maana hata katika Katiba Inayopendekezwa yametajwa na ndiyo maana tunasema ipigiwe kura ya ‘ndio’,” alisema.
 
Suluhu alisema anawashangaa watu wanaoupinga Muungano kwa madai kuwa huenda wana sababu zao kwani watanzania wengi bado wanaupenda na kuunga mkono.
 
Alitoa wito kwa watanzania kufika katika makumbusho hayo yaliyopo Posta jijini humo kwa nia ya kujifunza mambo mbalimbali juu ya Muungano huo ili wayajue na kuyaelewa.
 
“Njooni mjifunze mambo ya msingi juu ya Muungano wetu, wenzetu wa makumbusho wametenga siku saba kwa ajili yenu, mje mjifunze ili muuelewe vizuri muungano huu,” alitoa wito.
Mpekuzi blog

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.