Mchaka Zaidi

Friday, April 17, 2015

NDEGE AINA YA KWALE NAMNA ALIVYO NA UMAARUFU BAADA YA UTAFITI WA KUBAINI FAIDI NYINGI KATIKA MWILI WA BINADAMU.

Katika siku za hivi karibuni ndege aitwae kware ameanza kuwa ndege maarufu katika baadhi ya wafugaji katika nchi yetu na kwa wale ambao walikuwa wakiwawinda porini enzi na enzi kwa ajili ya kitoweo.

 

Watu bado wana imani kuwa ndege huyu hawezi kufungwa kama hatakimbia basi atajiua, lakini kwa wale wanaotaka kumfuga ndege huyu mdogo mwenye mayai matamu ya madoadoa wanaweza sasa inaweza kugeuka chanzo cha mapato na sehemu ya chakula bora kwa familia.

Mayai ya kware na yale ya kuku ingawa taarifa nyingi nilizopata kwenye mitandao na kwingineko inaonyesha tu kwa habari za watu waliopata kutumia mayai ya kware na kuona umuhimu wake katika afya.


Baadhi ya tovuti kuongelea tu kwamba mayai haya ni mazuri yanasaidia kwa afya bado kama watu wanaotaka kueleew inakuwa haikidhi haja kuamani tu ya kuwa yana saidia katika afya, yanasaidia watu walikuwa na matatizo mbalimbali ya kiafya wakiendelea vizuri.

 
Mayai ya Kwale ni chakula bora na sio dawa kama watu wengi waliotumia wakapata nafuu kwa yale waliokuwa yakiwasibu na wale waliokuwa na dhaifu nyingine katika mwili wakarejea afya maridhawa kwani haya mayai yana mchango mkubwa pia kama chakula bora.

Mwenyezi Mungu aliamua kuwapa wana waisrael kama chakula kwenye Kutoka 16:13 na mtumishi Daudi anakomelezea kwenye Zaburi 105:40. Sasa kwa kuwa siku zote najua kuwa Mungu hapingani na sayansi kitu wanasayansi wanachofanya nikungudua tu mambo ambayo Mungu ameyaweka kwahiyo ikabidi nitafute kisayansi sasa sisi tunaopenda kuoona na kufanya akili zetu zielewe maana ukielewa jambo kwenye akili yako ni rahisi kufanyia kazi.

Katika kutafuta nikasema pamoja na vyanzo vya wataalamu binafsi ningependa kupata vyanzo vilivyo vya kiserekali ambavyo wao hawana upande waliolalia maana hawa wataalamu binafsi wanaweza kuwa na ajenda zao.


Utafiti wa USDA (United State Department of Agriculture) unaonyesha tofauti za mayai haya kwa kina katika category 78 za nutrients zilizogawanya mayai ya kware yana vitu 31 zaidi ambayo ya kuku hayana kabisa wakati yale ya kuku ya kitu kimoja tu ambacho hakiko kwenye ya kware.

Vitamin K (phylloquinone) na katika hizo 45 vilivyobaki vya kware 42 viko juu na vingine hata mara mbili ya zile za kuku, wakati vya kuku ni 3 vitatu ambayo vimezidi vile vya kware. Angalia link hizo hapo chini kwa number kamili

Faida hizi zote tunaweza kupata kama watu wetu watajiingiza katika ufugaji wa ndege huyu ambaye anapatikana sehemu nyingi unaweza kuanza kidogo kidogo mpaka wakafikia mwengi,na kama unavyooana hapo juu unaweza kutengeneza banda rahisi la mbao laini na wafu na kuanzia hapo, ila wawapo wadogo waweke kwenye box na kuwawekea taa kama ufanyavyo kuku.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.