Mchaka Zaidi

Thursday, April 30, 2015

Taasisi Ya Kiislam Yatishia Kuandamana Nchi Nzima......Yaipa Serikali Siku 15 Kufungua Madrasa na Kuwaachia Huru Masheikh Waliokamatwa

 
Jumuiya na Taasisi za Kiisalam nchini, imetoa tamko na kuipa serikali siku 15 kabla ya kufanya maandamano nchi nzima kuelekea Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakidai kufunguliwa kwa madrasa zilizofungiwa kwa kuhusishwa na kutoa mafunzo ya ugaidi.

Vurugu Burundi: Mitandao ya Kijamii Ikiwemo Facebook,Twitter,Whatsapp Yafungwa

 
MAMLAKA nchini Burundi zimekata mawasiliano ya mitandao ya kijamii kupitia simu za mkononi, ambayo yamekuwa yakitumika kupanga maandamano ya kumpinga Rais Pierre Nkurunziza.
 

Sarafu ya Sh 500 YAHUJUMIWA....... Yanunuliwa kwa Sh. 2500 hadi 5000 ili Kutengeneza Mikufu, Benki Kuu Ya Tanzania (BoT) Yatoa Tamko

 
SARAFU mpya ya shilingi 500 inadaiwa kuhujumiwa na baadhi ya watu ambao huinunua kwa Sh 2,500 na baadaye kuiyeyusha kwa ajili ya kutengenezea mikufu ya fedha (silver).
 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Tarehe 30 April 2015



Diamond, Ali Kiba wachuana Tuzo za Watu

 


WANAMUZIKI mahiri wa muziki wa Bongo fleva nchini, Naseeb Abdul ‘Diamond Platinumz’ na Ali Kiba, ni miongoni mwa wasanii wanaochuana katika Tuzo ya Msanii Bora wa Kiume katika Tuzo za Watu 2015.
 

Yanga kuibeba Simba CAF?


BAADA ya watani zao wa jadi Yanga kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu vita ya kuwania kushiriki michuano ya kimataifa sasa mwakani imesalia kwa vigogo wengine wa soka nchini Simba SC na Azam FC.

Mbunge Bahi , Omary Badweli, Ashinda Kesi ya Kuomba RUSHWA

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemwachia huru Mbunge wa Jimbo la Bahi mkoani Dodoma, Omary Badweli, aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka mawili ya kuomba na kupokea rushwa kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Wilaya ya Mkuranga.

UKAWA Washindwa Kuafikiana.......NCCR Mageuzi Yawasilisha Hoja Ya Kujitoa, CUF Watoa Masharti Mazito

 
KIKAO cha viongozi wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kimeshindwa kuendelea baada ya baadhi ya wajumbe kushindwa kuafikiana kuhusu hoja iliyowasilishwa na Chama cha NCCR-Mageuzi, ya kutaka kujitoa kwenye umoja huo, imefahamika.
 

Godbless Lema Amshambulia Zitto Kabwe......Amtuhumu Kuikosesha CHADEMA Ushindi Mwaka 2010


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimewatoa hofu wanachama wake mkoani Shinyanga kikidai propaganda zinazoenezwa na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Bw. Zitto Kabwe, anayedai chama hicho kimepoteza mwelekeo si za kweli bali ni uongo.

Saturday, April 25, 2015

ACT-Tanzania Yabadili Jina

 
Chama kipya cha ACT-Wazalendo kinachoongozwa na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (pichani juu), kimebadili jina lake la awali la ACT-Tanzania.

Serikali Yaanza Tathmini Kero za Muungano

 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais( Muungano) Samia Hassan Suluhu amesema kero mbalimbali za Muungano zilizoibuliwa zimeanza kufanyiwa tathmini na Serikali.
 

Udampo wa Bidhaa za nje Anguko la Shilingi ya Tanzania

 
Shilingi ya Tanzania itaendelea kuporomoka kila mara endapo nchi itaendelea kutegemea bidhaa toka nje kwa kiwango kikubwa kuliko inavyozalisha ndani.
 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Tarehe 25 April 2015



Polisi Anusurika Kuuawa na Wananchi Wenye Hasira Kali Mkoani Morogoro jana Mchana


Askari mmoja wa jeshi la polisi ambao hutumia pikipiki kufanya doria, aliyejulikana kwa jina la Ramadhani, amenusurika  kuuawa  leo (jana)  mchana  na wananchi wenye hasira mjini Morogoro kwa kutuhumiwa kusababisha ajali ya dereva wa bodaboda ambaye aliparamia lori.
 

Afande Sele: Nikichaguliwa Kuwa Mbunge Nitakataa Posho na Mishahara Mikubwa


Mwana hip hop na Bongo Fleva nchini, Afande Sele, ameweka wazi kwamba hata kama atakuwa mwakilishi wa wananchi katika bunge la mwakani, hataweza kuacha kufanya muziki kwa kuwa ndiyo njia ya kumuingizia kipato.
 

CCM Wamjibu Dr. Slaa Kuhusu NEC......Wakanusha Kukisaidia Chama Kipya Cha ACT-Wazalendo



Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, amekanusha madai yaliyotolewa na  Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, kwamba Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeanza kuandikisha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika ngome za CCM na kueleza kuwa  huo ni upotoshaji mkubwa kwani Tanzania  nzima ni ngome ya chama hicho.

Wednesday, April 22, 2015

Breaking News: Watu 10 Wafariki Dunia Baada ya Basi la kampuni ya Unique Kugongana na Gari la Coca Cola



Habari  zilizotufikia  zinaarifu  kuwa  basi la Unique lenye namba za usajili T148 BKK likitokea jijini Mwanza kwenda Tabora limegongana uso kwa uso na lori la kampuni la Cocacola katika kijiji cha Ibingo kata ya Samuye Shinyanga.

Mapambano Bado Yanaendelea......Jana CHADEMA na ACT-Wazalendo Nusura Wakutane Uso Kwa Uso Nyumbani Kwa Baba wa Taifa. Vurugu Za Mnyika Ziligonga Mwamba Kwa Mara Nyingine


Mtoto wa Hayati baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Andrew Nyere, akiteta jambo na Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe na kuvaa kofia ya Chama cha ACT-Wazalendo wakati viongozi wa chama hicho walipofanya ziara kijijini Mwitongo Wilayani Butiama.

Mambo Yameiva: Mmiliki wa Gombe high School, Dkt Yared Fubusa Atangaza Nia Ya Kugombea Ubunge Jimbo La ZITTO KABWE Kwa Tiketi ya CHADEMA


Mwanzilishi na  Mkurugenzi wa Gombe school of Environment and Society (GOSESO) na mmiliki wa Gombe high school, Dkt Yared Fubusa ambaye pia ni kada wa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) ametangaza nia ya kugomba ubunge jimbo la Kigoma kaskazini kupitia chama hicho.

Sunday, April 19, 2015

Wema Sepetu: Niacheni nipumzike na mimi ni binadamu

 
Mwigizaji Wema Sepetu amewataka watu wanomsakama kwa maneno waache apumzike kufanya hivyo kwani yeye ni binadamu kama ilivyo kwa wengine na anaumia kama wanavyoumia wengine.
 

Watanzania Washika Silaha Afrika Kusini....Wajiandaa Kujihami Dhidi ya Mashambulizi ya Wenyeji

 
Raia wa Tanzania wanaoishi Afrika Kusini sasa wanadaiwa kushika silaha tayari kwa mapambo dhidi ya vikundi vya raia wa Taifa hilo vinavyoshambulia wahamiaji wa Kiafrika.
 

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili Ya Tarehe 19 April 2015

DSC01503

Dk.Mengi ashtushwa na tuhuma zinazodai kuwa ana nia ya kutaka kuiangusha serikali ya Rais Kikwete.

MWENYEKITI wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi, ametuhumiwa kutaka kuiangusha Serikali ya Rais Jakaya Kikwete na kumshughulikia baada ya kumaliza uongozi wake Oktoba, mwaka huu. 

CHADEMA wamtaka Rais kutokusaini Muswada wa sheria ya Uhalifu wa Mtandao


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimewataka wadau wa habari na taasisi mbalimbali, zikiwemo za kimataifa kuangalia kwa makini na kujadili baadhi ya vifungu vilivyopo katika muswada wa habari ili kuishawishi serikali kutousaini kwa kuwa unalenga kubana uhuru wa vyombo vya habari nchini.
 

Mtazame Hussein Machozi Kwa Mara ya Kwanza Akiongelea Tetesi za Yeye Kuwa Amefariki Dunia kwa Ajali ya Gari-BONGO FUSE

 
Juzi Kila Kona kwenye mitandao kulizuka habari kuwa Hussein Machozi Amefariki Dunia kitu ambacho kumbe hakikua Kweli ..
 

Watanzania Hatarini Ghasia za Afrika Kusini

Watanzania wanaoishi Afrika Kusini, wako hatarini kutokana na vurugu zinazofanywa na wenyeji wa nchi hiyo, dhidi ya wananchi wengine wa asili ya Afrika wanaoishi nchini humo.

Watoto 115 wanaswa wakipatiwa mafunzo Dodoma

 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma limeviweka chini ya ulinzi na kuvifanyia uchunguzi vituo vitatu vilivyokusanya watoto 115 kutoka mikoa 13 nchini kwa lengo la kuwapatia mafunzo ya dini ya Kiislamu.
 

Friday, April 17, 2015

Tamko la Waziri Chikawe Kuzifuta Taasisi za Kidini na Kiraia Zinazojihusisha Na Siasa Lapingwa Kila Kona.......Yadaiwa ni Udikteta na Aibu kwa Demokrasia


Wasomi, wanasiasa, viongozi wa dini na wananchi katika maeneo mengi nchini, wamepinga vikali tishio la Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe, la kuzifuta taasisi za kijamii na kidini na kueleza kuwa amekurupuka, hakushauriwa na kushindwa kufuata misingi ya demokrasia na Katiba ya nchi.

NDEGE AINA YA KWALE NAMNA ALIVYO NA UMAARUFU BAADA YA UTAFITI WA KUBAINI FAIDI NYINGI KATIKA MWILI WA BINADAMU.

Katika siku za hivi karibuni ndege aitwae kware ameanza kuwa ndege maarufu katika baadhi ya wafugaji katika nchi yetu na kwa wale ambao walikuwa wakiwawinda porini enzi na enzi kwa ajili ya kitoweo.

 

Thursday, April 16, 2015

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamis ya April 16,2015



'Magaidi' 10 Wakamatwa Msikitini Wakiwa na Milipuko, Sare za jeshi na Bendera ya Al Shabaab

 
Watu 10 wanashikiliwa na polisi mkoani Morogoro baada ya kukamatwa msikitini wakiwa na milipuko 30, sare za jeshi na bendera nyeusi inayodaiwa kutumiwa na kundi la wapiganaji wa Al Shabaab wa nchini Somalia.

Utata Wa Nay Wa Mitego na Siwema Umekwisha Baada ya Majibu ya DNA Kutoka


Baada ya utata mzito kutawala kwenye vyombo vya habari juu ya uhalali wa mtoto wa Mbongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ kwa mzazi mwenzake Siwema Edson, hatimaye kipimo cha vinasaba (DNA) kimetoka na kumaliza ubishi kwamba mtoto huyo aitwaye Curtis ni damu halisi ya msanii huyo.

Wednesday, April 15, 2015

Habari zilizopo Katika Magazeti ya Leo


Zitto Kabwe: Sitaki kulumbana na CHADEMA


Kiongozi wa chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe amesema hawezi kulumbana na viongozi wa chama chake cha zamani cha Chadema kwa kuwa anachofanya sasa ni kutafuta wanachama wa chama chake kipya. 
 

Radi Yaua Mwalimu na Wanafunzi 6 Kigoma


Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya mkoa wa Kigoma,Maweni  akiongeza na Waandishi wa habari juu ya tukio la radi lililotokea hivi punde na kuuwa watu 8

Kamanda Mpinga: Madereva Waliosababisha Ajali Kwa Uzembe Kufutiwa Leseni Zao

 
Kamanda wa Polisi wa kikosi cha usalama Barabarani Mohammed Mpinga,akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani ofisini kwake jijini Dar es Salaam  jana.

Lipumba: Siku Ya Uchaguzi Mkuu Itatangazwa Na NEC Na Si Vinginevyo



 
Mwenyekiti wa taifa wa Chama  cha Wananchi (CUF),Profesa   Ibrahim Lipumba akizungumza na baraza la uongozi wa chama hicho (hawapo pichani) iliyofanyika Makao Makuu ya Chama hicho jijini Dar es Salaam, wapili kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad, kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Zanzibar,Nassor Ahmed na kushoto ni makamu Mwenyekiti wa chama cha Wananchi (CUF) Taifa,Duni Haji.

Tuesday, April 14, 2015

Huyu Ndo Mtanzania Anayetuhumiwa Kwa Ugaidi Kenya.....Jana Alifikishwa Mahakamani Chini Ya Ulinzi Mkali

 
Mtanzania anayedaiwa kuhusika katika shambulizi la kigaidi lililoua watu 148 katika Chuo Kikuu cha Garissa – Kenya, Rashid Charles Mberesero, jana alifikishwa mahakamani na kuwekwa kizuizini kwa mwezi mmoja wakati polisi wakiendelea kukusanya ushahidi dhidi yake.
 

AJIRA MPYA KWA WALIMU

 
Serikali imesema ajira za walimu wapya zitaanza rasmi Mei Mosi, mwaka huu huku ikiweka wazi kuwa walimu hao wasitegemee kupangiwa katika maeneo ya majiji, manispaa na miji.
 

JWTZ iliandaa mabasi 300 kuukabili mgomo wa madereva


Kutokana na mgomo wa madereva wa mabasi ya abiria nchi nzima uliofanyika Ijumaa iliyopita, Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lilikuwa limeshaandaa mabasi 300 ambayo yangetumika kusafirisha abiria, imebainika.
 

Nape awajibu wanaoishinikiza CCM... kuhusu ratiba ya uchaguzi




 
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, amesema chama hicho hakitaendeshwa kwa mashinikizo ya watu wanaotaka kitangaze haraka ratiba ya uteuzi wa wagombea wake kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao. 

Madereva Wa Mabasi Kugoma Tena April 18 Iwapo Sharti la Mikataba Halitatimizwa......Msimamo huo Walimweleza Zitto Kabwe






 


















Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Bw. Zitto Kabwe, ameitaka Serikali kuhakikisha madereva wote wa magari ya mizigo na mabasi ya abiria, wanapewa mikataba ya ajira kabla ya Aprili 17, mwaka huu.

Lowassa atajwa tena.....Kada mkongwe atoa ya moyoni juu ya kifungo chake.












































Wakati Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikiendelea kutafakari jinsi kitakavyompata mgombea wake atakayepeperusha bendera ya urais katika uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu,

Serikali Yapata Kigugumizi Shule za Sekondari Kufungwa Kutokana na Kukosa Chakula!!!



Kizungumkuti kimezidi kujitokeza katika suala la kufungwa kwa shule za sekondari za bweni za serikali kwa kile kinachoelezwa ni ukosefu wa chakula kutokana na wazabuni kugoma, baada ya serikali kutoa tamko ikieleza kuwa kuwa imelipa fedha za wazabuni hadi Machi, mwaka huu.