Jumuiya na Taasisi za Kiisalam nchini, imetoa tamko na kuipa serikali siku 15 kabla ya kufanya maandamano nchi nzima kuelekea Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakidai kufunguliwa kwa madrasa zilizofungiwa kwa kuhusishwa na kutoa mafunzo ya ugaidi.

MAHAKAMA
ya Hakimu Mkazi Kisutu imemwachia huru Mbunge wa Jimbo la Bahi mkoani
Dodoma, Omary Badweli, aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka mawili ya
kuomba na kupokea rushwa kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Wilaya ya Mkuranga.






| Mtoto wa Hayati baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Andrew Nyere, akiteta jambo na Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe na kuvaa kofia ya Chama cha ACT-Wazalendo wakati viongozi wa chama hicho walipofanya ziara kijijini Mwitongo Wilayani Butiama. |

MWENYEKITI wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi, ametuhumiwa kutaka
kuiangusha Serikali ya Rais Jakaya Kikwete na kumshughulikia baada ya
kumaliza uongozi wake Oktoba, mwaka huu.

Watanzania
wanaoishi Afrika Kusini, wako hatarini kutokana na vurugu zinazofanywa
na wenyeji wa nchi hiyo, dhidi ya wananchi wengine wa asili ya Afrika
wanaoishi nchini humo.






