Mchaka Zaidi

Thursday, May 21, 2015

Rais Pierre Nkurunziza Asogeza Mbele Uchaguzi wa Wabunge Kwa Siku 10



Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza amesogeza mbele uchaguzi wa wabunge kwa siku 10 hadi Juni 5 mwaka huu kufuatia jaribio la mapinduzi.

Msemaji wa Rais, Willy Nyamitwe ameliambia Shirika la Habari la AFP kuwa kufuatia jaribio la mapinduzi la wiki iliyopita na vurugu zilizofuatia ni bora kusogeza mbele uchaguzi huo kwa muda.
 
"Uchaguzi huo wa wabunge ulikuwa umeratibiwa kufanyika Mei 26 mwaka huu lakini sasa inatubidi kuusogeza mbele mpaka Juni 5 mwaka huu ili kuwasikiza washirika wetu wa kimataifa pamoja na tume ya uchaguzi ambayo pia inatumia muda huo kutatua maswali yaliyoulizwa na vyama vya upinzani" alisema Nyamitwe.

Mpaka sasa tarehe rasmi ya uchaguzi wa urais uliopangwa kufanywa Juni 26 mwaka huu bado haijabadilika na nia ya Rais Nkurunziza kuwania urais kwa muhula wa tatu ipo palepale.
Chanzo:
Mpekuzi blog

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.