Mchaka Zaidi

Monday, July 27, 2015

Lowassa na UKAWA , NEC kuhusu Kampeni za Magufuli? ACT Wazalendo na UKAWA? (Audio)

mr


Magazeti ya Tanzania July 27 2o15 na headlines zake kubwakubwa yako mtaani, hapa ninazo chache kwenye zile zilizobebwa leo.
Lowassa akoleza joto Urais UKAWA, asubiriwa kujiunga CHADEMA, ACT Wazalendowatamba kusimama kivyaovyao Uchaguzi 2015, CUF yabariki mgombea Urais UKAWA naObama amaliza ziara yake ya siku 3 nchini Kenya.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC yadai kuwa Mgombea Urais kupitia CCM Dk. John Magufuli anakiuka sheria na kanuni za Uchaguzi Mkuu kwa kuanza kampeni kabla ya wakati.
Changamoto za BVR bado zinaendelea kuibuka Dar, lengo la kusajili watu Mil.2 linazidi kutia mashaka baada ya kasoro kadhaa zinazoendelea kujitokeza.
Zitto Kabwe asema kuwa Chama cha ACT Wazalendo kitasimama chenyewe kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu na hakitaungana na UKAWA.
Rais Barack Obama amaliza ziara yake ya Siku 3 nchini Kenya, akumbushia changamoto alizozipata kabla ya kuwa Rais ikiwemo kuibiwa begi Airport ya Jomo Kenyatta.
Stori zote kwenye Uchambuzi wa #PowerBreakfast nilirekodi na nimekusogezea hapa.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.