Mchaka Zaidi

Tuesday, March 31, 2015

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Tarehe 31 March 2015



Kaka Yake Gwajima Amtaka Amuombe Radhi Pengo.



Kaka wa Askofu wa kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima aitwaye Methusela Gwajima amemtaka mdogo wake kwenda kumuomba radhi Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki Dar es Salaam Mhadhama Polycarp Kadinali Pengo kwa kutoa lugha ya kumkashifu.
 

Watu Watano Wajeruhiwa Vibaya baada ya Kuangukiwa na Kifusi Cha Ukuta wa Jengo la Ghorofa 7 Jijini Mwanza.



Watu watano katika Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza wamenusurika kifo baada ya kuangukiwa na kifusi wakati wakiwa kwenye maandalizi ya kujenga jengo lililotegemewa kuwa na ghorofa saba, eneo la Nyerere Road,   jana majira ya saa sita mchana.
 

Sunday, March 29, 2015

Urais 2015: Lowassa Aongoza, Mwingulu Nchemba Ang'ara Kama Kijana Anayekubalika Zaidi.



Taasisi isiyo ya kiserikali ya Positive Thinkers Tanzania imetoa ripoti yake ya utafiti kuhusu mwanasiasa anayekubalika zaidi na wananchi katika nafasi ya Rais ajaye.