Mchaka Zaidi

Thursday, May 7, 2015

RAIS WA BURUNDI PIERRE NKURUNZIZA HATAGOMBEA TENA URAIS.

http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/2705586/highRes/1005433/-/maxw/600/-/d89d2d/-/pierre.jpgRais wa Burundi Pierre Nkurunziza amewaambia mawaziri wa Afrika Mashariki kwamba endapo atachaguliwa kuiongoza nchi hiyo mwezi June mwaka huu kwa muhula wa tatu basi itakuwa ni kipindi cha ukomo wa yeye kuendelea kusalia madarakani ,msemaji wa serikali ya Burundi Gervais Abayehorwa amesema hayo mapema Jumatano.

Profesa Lipumba Aieleza Mahakama ya Kisutu kuwa Polisi WALIMPIGA, Akana Kufanya Maandamano

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kuwa, hawakufanya maandamano wala kupata barua ya zuio badala yake alipigwa na polisi.

Zitto Kabwe Afunguka Kuwa Alipofukuzwa CHADEMA Alitamani Kujiunga NCCR-Mageuzi......Kazungumzia Pia Anakotoa Pesa za Kufanya Mikutano

 
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe amefunguka na kusema kuwa alipofukuzwa Uanachama katika chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) alitamani kujiunga na Chama Cha NCCR-Mageuzi kwani ndicho chama ambacho kilikuwa  kinaendana na itikadi yake anayoifuata na kuiamini ambayo ni itikadi ya Ujamaa.
 

Monday, May 4, 2015

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Tarehe 4 May 2015



MGOGORO: Kanisa la Moravian Wakataa Jimbo jipya.


KANISA la Moravian Jimbo la Mashariki limeitaka Serikali iangalie upya uamuzi wake wa kuruhusu mgawanyiko wa kanisa hilo kwa kuruhusu usajili wa Jimbo lingine ili kuepusha uvunjifu wa amani.
 

Uchambuzi wa Zitto Kabwe: Yaliyojificha Kuporomoka Kwa Shilingi Dhidi ya Dola ya Marekani

 
Na Zitto Kabwe,Mpekuzi.
Katika ukurasa wangu wa facebook mnamo tarehe 25 Aprili 2015 niliandika kuhusu sababu za shilingi kuporomoka thamani na majawabu ya namna ya kurejesha thamani halisi ya sarafu yetu.